Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 2 Water and Irrigation Wizara ya Maji 37 2022-09-14

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. ALEXANDER P. MNYETI K.n.y. MHE. DAVID M. KIHENZILE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapeleka maji katika Kata ya Mwabuki?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI K.n.y. WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Alexander Pastory Mnyeti Mbunge wa Jimbo la Misungwi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Kata ya Mwabuki ina jumla ya vijiji sita vya Lubuga, Mhungwe, Mabuki, Mwagagala, Mwanangwa na Ndinga. Kwa sasa vijiji hivyo vinapata huduma ya maji kupitia visima vya pampu za mkono ambapo hali ya huduma ya maji ni asilimia 39.

Mheshimiwa Spika, katika kuboresha huduma ya maji Kata ya Mwabuki katika mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali imekamilisha usanifu wa mradi wa maji kutoka bomba kuu la KASHWASA kupeleka katika vijiji vyote vya Kata ya Mwabuki. Kwa sasa taratibu za manunuzi zinaendelea na ujenzi unatarajiwa kuanza mwezi Desemba, 2022 na kukamilika mwezi Desemba, 2023. Kukamilika kwa mradi huo kutaongeza huduma ya upatikanaji wa maji kutoka asilimia 39 hadi kufikia asilimia 100.