Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 2 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 35 2022-09-14

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SUBIRA K. MGALU aliuliza: -

Je, ni lini Hospitali ya Rufaa Tumbi na Hospitali za Wilaya za Mkoa wa Pwani zitapokea vifaa tiba ikiwa ni sehemu ya fedha za kupambana na UVIKO-19?

Name

Ummy Ally Mwalimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tanga Mjini

Answer

WAZIRI WA AFYA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Subira Khamis Mgalu, Mbunge Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani - Tumbi imeshapokea vifaa tiba 74 kati ya 77 vilivyoagizwa kwa fedha za kupambana na UVIKO-19, hii ni sawa na asilimia 94 ya vifaa vyote vilivyoagizwa ikiwemo mashine ya CT Scan. Kazi ya kusimika vifaa hivi inaendelea na inatarajiwa kukamilika mwezi Oktoba, 2022.

Mheshimiwa Spika, aidha, kwa upande wa Hospitali za Wilaya, ujenzi wa majengo ya huduma za dharura yaani EMD na majengo ya huduma za wagonjwa waliopo kwenye uangalizi maalum yaani ICU unaendelea. Hivyo vifaa tiba kwa ajili ya hospitali hizi vitafikishwa mara baada ya ujenzi kukamilika.