Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 2 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 27 2022-09-14

Name

Njalu Daudi Silanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Itilima

Primary Question

MHE. STANSLAUS H. NYONGO K.n.y. MHE. NJALU D. SILANGA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya kutoka Sibiti – Kisesa – Itilima – Bariadi
– Salama - Sayaka hadi Kisamba kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Njalu Daudi Silanga Mbunge wa Itilima kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ya kutoka Sibiti hadi Mwandoya Junction ama Loboko ni sehemu ya barabara ya Karatu – Mbulu – Hydom – Sibiti – Lalago – Maswa yenye urefu wa kilometa 389 ambayo imepangwa kujengwa kupitia utaratibu wa Engineering, Procurement, Construction & Financing (EPC + F).

Mheshimiwa Spika, sehemu ya Mwandoya Junction hadi Kisesa – Itilima – Bariadi yenye urefu wa kilometa 100, kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina inaendelea na sehemu ya kutoka Bariadi – Salama hadi Magu kupitia Ng’haya (kilometa 76) ipo katika hatua ya manunuzi ya kumpata Mhandisi Mshauri kwa ajili ya kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina. Ahsante.