Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 3 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 47 2022-09-15

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya zege ya kilometa tatu kwenye Mlima Magara katika Jimbo la Mbulu Mjini?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu la Mheshimiwa Zacharia Paulo Issaay, Mbunge wa Mbulu Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, eneo korofi na hatarishi katika Mlima Magara lina urefu wa kilometa saba. Kati ya hizo kilometa saba, Serikali imekamisha ujenzi kwa kiwango cha zege kilometa nne. Katika Mwaka wa Fedha 2022/2023, Serikali itaendelea na ujenzi kwa kiwango cha zege kwa kiasi cha kilometa moja. Kilometa mbili zilizobaki zitaendelea kujengwa kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha. Ahsante.