Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 3 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 43 2022-09-15

Name

Emmanuel Lekishon Shangai

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Primary Question

MHE. EMMANUEL L. SHANGAI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itawapatia Vitambulisho vya Taifa na vyeti vya kuzaliwa wananchi wa Kata za Ololosokwan, Soitsambu na Enguserosambu Ngorongoro?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Emmanuel Shangai Mbunge wa Jimbo la Ngorongoro kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, hadi kufikia mwezi Agosti 2022 jumla ya wananchi 84,637 katika Wilaya ya Ngorongoro wametambuliwa na kusajiliwa. Namba za Utambulisho 61,237 ambayo ni sawa na asilimia 72.3 ya wananchi wote waliotambuliwa na kusajiliwa zimezalishwa na kugawiwa kwa wananchi. Aidha, jumla ya vitambulisho 46,997 ambayo ni sawa na asilimia 76.7 ya namba za utambulisho tajwa vimezalishwa pamoja na kugawiwa kwa wananchi wa Wilaya ya Ngorongoro.

Mheshimiwa Spika, usajili na utambuzi wa wananchi na uzalishaji na ugawaji Vitambulisho vya Taifa ni kazi endelevu. Hivyo, Mamlaka itaendelea na usajili wa wananchi wanaokidhi vigezo kupitia ofisi za usajili wa wilaya pamoja na kuzalisha na kugawa Vitambulisho vya Taifa kwa wananchi kupitia katika kata zote.

Mheshimiwa Spika, usajili na utoaji wa vyeti vya kuzaliwa bila malipo unaendelea katika vituo vyote vinavyotoa huduma ya afya ya mama na mtoto pamoja na vituo vya kata.