Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 3 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 39 2022-09-15

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU K.n.y. MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za watumishi waliohamishiwa Halmashauri mpya Nzera?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Musukuma Joseph Kasheku Mbunge wa Jimbo la Geita Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali ilitenga kiasi cha Shilingi Milioni 150 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba ya Mkurugenzi katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita, ambapo ujenzi wa nyumba hiyo unaendelea na upo katika hatua ya upauaji.

Mheshimiwa Spika, mwaka wa fedha 2022/2023 Halmashauri ya Wilaya ya Geita imetengewa kiasi cha Shilingi Milioni 240 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba mbili (2) za Wakuu wa Idara.

Mheshimiwa Spika, Serikali inaielekeza Halmashauri ya Wilaya ya Geita na Halmashauri nyingine kote nchini zenye upungufu wa nyumba za watumishi kuendelea kutenga bajeti za mapato ya ndani kila mwaka ili kutatua changamoto za upungufu wa nyumba za watumishi. Ahsante.