Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 4 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 49 2022-09-16

Name

Jackson Gedion Kiswaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. JACKSON G. KISWAGA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapeleka fedha za kujenga Vituo vya Afya katika Kata ya Lyamugungwe na Kihanga?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais,TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jackson Gedion Kiswaga, Mbunge wa Jimbo la Kalenga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali katika mwaka wa fedha 2021/2022 ilipeleka Shilingi bilioni 1.3 kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya vitatu katika Wilaya ya Iringa. Aidha, katika mwaka wa fedha 2022/2023 Halmashauri ya Wilaya ya Iringa kupitia mapato ya ndani imetenga Shilingi milioni 400 kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya Magulilwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kati ya Kata ya Lyamungungwe na Kihanga, Serikali itajenga Kituo cha Afya cha kimkakati katika Kata ya Kihanga ambayo itatengewa fedha kwenye bajeti ya mwaka 2024/2025. Ahsante.