Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 5 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 75 2022-09-19

Name

Michael Mwita Kembaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Mjini

Primary Question

MHE. MICHAEL M. KEMBAKI aliuliza: -

Je, kwa nini darasa la saba wanafanya mtihani wa Taifa mwezi Septemba, wakati mtaala unaelekeza masomo yakamilike mwisho wa mwaka?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, napenda sasa kujibu swali la Mheshimiwa Mwita Kembaki Michael, Mbunge wa Tarime Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, mtaala wa elimu unaelekeza mwanafunzi kutumia siku 194 za mwaka kwa masomo. Aidha, mtaala wa elimu pamoja na masuala mengine umezingatia muda wa kufanyika kwa mitihani ya ndani na ile ya Kitaifa. Hivyo, kukamilika kwa ufundishaji na ujifunzaji wa maudhui ya muhtasari kwa darasa la saba hutegemea zaidi mpango kazi wa Mwalimu. Kwa msingi huo, hadi kufika mwezi wa Septemba walimu wa darasa la saba hupaswa kuwa wamekamilisha kufundisha mada zilizobainishwa katika muhtasari ili kutoa nafasi ya ufanyikaji wa mitihani ya Kitaifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ufanyikaji wa mitihani ya kitaifa ya darasa la saba mwezi Septemba unasaidia kutoa nafasi kwa zoezi la usahihishaji na utoaji wa matokeo kwa wakati ili kutoa nafasi kwa wazazi na walezi kufanya maandalizi ya kuwawezesha watoto wao kujiunga na masomo ya ngazi nyingine za elimu ambapo masomo yanaanza Januari mwaka unaofuata. Ninakushukuru.