Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 5 Youth, Disabled, Labor and Employment Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu 68 2022-09-19

Name

Bonnah Ladislaus Kamoli

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Segerea

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI K.n.y. MHE. BONNAH L. KAMOLI aliuliza: -

Je, nini mpango wa kuhakikisha Madereva wa magari ya abiria na mizigo wanapewa mikataba ya kazi ili kupata mafao na Bima za Afya?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA NA VIJANA (MHE. PASCAL P. KATAMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bonnah Ladislaus Kamoli, Mbunge wa Segerea, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeendelea kusimamia Sheria za Kazi na kuwahimiza waajiri wote nchini kuwapatia wafanyakazi wao mikataba ya ajira kwa kuwa hili ni takwa la kisheria na ni haki ya wafanyakazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuhimza hili Serikali ilitoa tamko na maagizo kwa wamiliki wa mabasi na malori tarehe 12 Juni, 2022 na tarehe 22 Julai, 2022, kwamba ifikapo tarehe 30 Agosti, 2022, wafanyakazi madereva wote wawe wamepewa mikataba kwa mujibu wa sheria.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kutoa taarifa katika Bunge lako Tukufu kuwa waajiri wengi wametekeleza na baadhi bado wanaendelea kutekeleza mikataba hiyo kwa ajili ya kuwapatia madereva, lakini pia wafanyakazi wote katika sekta rasmi nchini. Aidha, Ofisi imejipanga na inaendelea kufanya ukaguzi maalum katika Sekta ya Usafirishaji na kuchukua hatua stahiki kwa waajiri wanao kiuka takwa hilo la kutoa mikataba kwa wafanyakazi madereva na Sekta nyingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kwa kutambua na kulinda haki za wafanyakazi madereva, imeweka utaratibu wa kukaa Vikao vya Mashauriano na Majadiliano na Viongozi wa Vyama vya Wamiliki wa Vyombo vya Usafirishaji (Malori na Mabasi) pamoja na Viongozi wa Vyama vya Wafanyakazi Madereva kwa lengo la kupeana taarifa kuhusu changamoto zinazowakabili madereva na kuzitafutia ufumbuzi. Aidha, utaratibu huu ni endelevu.

Mheshimiwa Mwenyekiti mbali na kaguzi hizo, nitoe rai na kumwomba Mheshimiwa Mbunge na Watanzania wote kutoa taarifa endapo watapata taarifa za kutokuwepo kwa mwajiri katika sekta hii ambaye bado hajatekeleza maagizo haya ya Serikali kwa kutoa mikataba ya ajira kwa wafanyakazi madereva, hatua stahiki zitaendelea kuchukuliwa pia kwa mujibu wa sheria kwa kutambua kwamba sekta hii ni muhimu na ina mchango mkubwa katika uchumi wa nchi yetu. Ahsante.