Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 7 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 113 2022-09-21

Name

Maimuna Ahmad Pathan

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MAIMUNA A. PATHAN aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itabadili utaratibu kuwataka wavuvi wanaotumia ring net kutoruhusiwa kuvua mchana na kuvua chini ya mita 50?

Name

Mashimba Mashauri Ndaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Magharibi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII K.n.y. WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, kwa niaba ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi naomba kujibu swali la Mheshimiwa Maimuna Ahmad Pathan, Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, matumizi ya wavu wa ring net wakati wa usiku yanawezesha kuvua samaki wanaolengwa yaani dagaa pekee na kupunguza uwezekano wa kukamata samaki wasiolengwa yaani by-catch. Aidha, matumizi ya wavu wa ring net kwenye kina cha mita 50 wakati wa maji kupwa kwa upande wa baharini na katika umbali wa mita 1,000 kutoka ufukweni kwenye visiwa na rasi kwa upande wa Ziwa Tanganyika yanawezesha kuwa na uvuvi endelevu kwa kutovua samaki wachanga na kutosababisha uharibifu wa maeneo ya mazalia, makulia na malisho ya samaki.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeendelea kutoa elimu kwa wavuvi pamoja na wadau wa uvuvi kudhibiti matumizi ya zana haramu katika shughuli za uvuvi ikiwemo matumizi ya ring net kwenye kina cha maji chini ya mita 50 na wakati wa mchana ili kuwa na uvuvi endelevu. Hivyo, kupitia Bunge lako tukufu; Serikali inatoa wito kwa jamii za wavuvi kuendelea kuzingatia sheria za nchi katika kulinda rasilimali za uvuvi kwa manufaa ya sasa na ya kizazi kijacho.