Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 7 Investment and Empowerment Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 109 2022-09-21

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. DAVID M. KIHENZILE aliuliza: -

Je, kwa miaka kumi ni wawekezaji wangapi wa nje walionesha nia ya kuwekeza na kufanikiwa na upi mkakati kwa ambao hawajafanikiwa?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara napenda kujibu swali la Mheshimiwa David Mwakiposa Kihenzile, Mbunge wa Jimbo la Mufindi Kusini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kupitia Kituo cha Uwekezaji (TIC) jumla ya miradi 4,543 ilisajiliwa katika kipindi cha miaka kumi kuanzia mwaka 2012 hadi mwaka 2021 ambapo mitaji yenye thamani ya dola za Marekani bilioni 53.1 ilitarajiwa kuwekezwa na kutoa ajira 654,260. Kati ya miradi hiyo, miradi 3,304 ilitekelezwa sawa na asilimia 72.7 ya miradi yote iliyosajiliwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea kuweka mikakati mbalimbali ya kufanikisha uwekezaji ikiwemo kuimarisha matumizi ya TEHAMA, dirisha moja la kuhudumia wawekezaji, kuboresha na kujenga miundombinu wezeshi, vivutio vya kikodi na visivyo vya kikodi na kutenga maeneo kwa ajili ya wawekezaji. Nakushukuru.