Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 7 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 105 2022-09-21

Name

Halima James Mdee

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HALIMA J. MDEE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali italipa madai ya shilingi trilioni 7.91 ya watoa huduma kama yalivyoripotiwa kwenye ripoti ya CAG 2021?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Halima James Mdee, Mbunge Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, deni la shilingi trilioni 7.91 linajumuisha madeni ya wafanyakazi na watoa huduma kwa mashirika ya umma 71. Ili kuhakikisha madeni hayo yanalipwa na kudhibiti uzalishaji wa madeni mapya, mashirika yote ya umma yameelekezwa kuendelea kulipa kwa haraka iwezekanavyo na kuandaa mkakati wa kukabiliana na madeni na kuwasilisha Ofisi ya Msajili wa Hazina.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mkakati huo, kila taasisi inatakiwa kuonesha namna itakavyodhibiti uzalishaji wa madeni mapya na kulipa madeni yaliyopo. Lengo ni kuhakikisha kuwa kiwango cha madeni kinafikia asilimia mbili ya jumla ya bajeti ya mashirika ya umma ifikapo mwaka 2025. Aidha, Ofisi ya Msajili wa Hazina na Idara ya Usimamizi wa Bajeti ya Serikali itatumia mkakati huo katika uchambuzi na uidhinishaji wa mapato na matumizi ya kila mwaka. Ahsante.