Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 7 Youth, Disabled, Labor and Employment Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu 95 2022-09-21

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. HUSNA J. SHEKIBOKO K.n.y. MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza: -

Je, kuna mkakati gani wa kurasimisha vijana waliopata ujuzi nje ya mfumo rasmi?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA NA VIJANA (MHE. PATROBAS P. KATAMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mussa Ramadhani Sima, Mbunge wa Singida Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inao mkakati kupitia Mpango wa Taifa wa maendeleo wa miaka mitano wa kurasimisha ujuzi uliopatikana nje ya mfumo rasmi wa mafunzo kwa vijana 100,000 ifikapo mwaka 2025/2026. Aidha, katika utekelezaji wake hadi kufikia Juni, 2022 kupitia Programu ya Taifa ya Kukuza Ujuzi jumla ya vijana wapatao 22,296 (kike 3,349 na kiume 18,947) kutoka mikoa yote ya Tanzania Bara wamerasimishwa ujuzi ikiwemo Singida zaidi ya watu 1,138.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunazo fani kumi zinazohusika katika urasimishaji ambazo ni uashi, useremala, ufundi magari (makenika), upishi na uhudumu wa hoteli, baa na migahawa, ufundi bomba, unyooshaji bodi za magari, umeme wa majumbani; ushonaji nguona uchomeleaji vyuma. Aidha, kutokana na manufaa wanayoyapata vijana, katika mwaka wa fedha 2022/2023 jumla ya vijana 18,445 (wa kiume 13,873 na wa kike 4,572) wamejitokeza na kukuziwa uchuzi na kuchukua fomu kwa ajili ya kurasimishwa ujuzi wao kupitia programu hii ambapo taratibu zinakamilishwa ili waweze kupatiwa fursa hiyo. Ahsante.