Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 8 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 128 2022-09-22

Name

Neema Gerald Mwandabila

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA G. MWANDABILA aliuliza: -

Je, nini mkakati wa Mahakama kutoa hukumu ya pande mbili hasa mtuhumiwa anaposhinda kesi kuepuka usumbufu kufungua kesi mpya ya kulipwa fidia?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Neema Mwandabila, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa kanuni na taratibu za madai ya fidia, kuachiwa huru kwa mshtakiwa katika shitaka la jinai hakumpi haki ya moja kwa moja ya kulipwa fidia. Ili mshtakiwa aweze kulipwa fidia kutokana na kushinda shauri la jinai, ni lazima athibitishe Mahakamani kwamba mashitaka dhidi yake yalikuwa ya hila; na kwamba hakukuwa na sababu za msingi za kumshtaki. Kuachiwa pekee kwa mshtakiwa katika shitaka la jinai hakumaanishi mashtaka dhidi yake yalikuwa ya hila na waliomshitaki hawakuwa na sababu ya kuamini alitenda kosa.

Mheshimiwa Spika, kifungu cha 345(2) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai kinaipa mamlaka Mahakama kutoa amri ya mtuhumiwa aliyeshinda shauri lake la jinai kulipwa gharama za shauri iwapo shauri hilo liliendeshwa na Mwendesha Mashtaka wa Kujitegemea (Private Prosecutor).