Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 8 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 114 2022-09-22

Name

Timotheo Paul Mnzava

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itakarabati Kituo cha Afya Bungu Wilayani Korogwe?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Timotheo Paul Mzava, Mbunge wa Jimbo la Korogwe Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Kituo cha Afya Bungu ni kikongwe, chakavu na kipo kwenye eneo finyu. Serikali imefanya tathmini na kuweka mpango wa kujenga kwa awamu Kituo cha Afya kipya kwa gharama ya shilingi milioni 400.

Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe katika mwaka wa fedha 2023/2024 itatenga kutoka mapato ya ndani shilingi milioni 100 kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya cha Bungu. Aidha, Halmashauri itaendelea kutenga fedha kila mwaka kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa Kituo hicho. Ahsante.