Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 9 Water and Irrigation Wizara ya Maji 152 2022-09-23

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kuvuna maji katika Mji wa Itigi?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante, kwa niaba ya Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Yahaya Omary Massare, Mbunge wa Manyoni Magharibi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali inaendelea na ukarabati wa mabwawa mawili ya Rungwa na Muhanga yenye thamani ya zaidi ya milioni 460 yenye ukubwa wa kati katika Wilaya ya Manyoni ili kuongeza uvunaji wa maji ya mvua yatakayonufaisha wananchi katika Wilaya hiyo.