Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 9 Works, Transport and Communication Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari 148 2022-09-23

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: -

Je, lini minara ya mawasiliano itajengwa katika Kata za Endanywish, Endagulda, Gidurdagaw, Yaeda Ampa, Hayeda na Endanilay?

Name

Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Answer

WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Flatei Gregory Massay, Mbunge wa Mbulu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kKuna mnara umejengwa katika kata ya Bashay kijiji cha Bashay kwa lengo la kutoa huduma katika kijiji cha Bashay na baadhi ya maeneo ya Yaeda Ampa. Hata hivyo, baada ya ujenzi wa mnara kukamilika, bado ilionekana kuwa Vijiji vya Arri na Hayeseng kutoka Kata ya Yaeda Ampa bado havipati huduma nzuri ya mawasiliano na hivyo viliingizwa katika orodha ya miradi ya Tanzania ya Kidigitali ambapo zabuni ya mradi huu inatarajiwa kutangazwa hivi karibuni mara idhini ya benki itakapotolewa.

Mheshimiwa Spika, Aidha, Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) imeziingiza Kata za Endahagichan yenye Vijiji vya Endadubu, Miqaw na Endahagichan, Kata ya Eshkesh yenye Vijiji vya Domanga na Endagulda, kata ya Geterer yenye Vijiji vya Magong na Mewada, Kata ya Haydarer yenye Kijiji cha Gidbiyo, Kata ya Masqaroda yenye Kijiji cha Harbanghet, na Kata ya Yaeda Chini yenye Kijiji cha Endajachi katika mradi wa Tanzania ya Kidijitali ambao kama nilivyosema zabuni yake inatarajiwa kutangazwa hivi karibuni. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa Kata za Endanywish, Endagulda, Gidurgadaw, Hayeda na Endanilay tathmini ilifanyika na maeneo hayo yalionekana yana changamoto za upatikanaji wa huduma za mawasiliano na hivyo yataingizwa katika orodha ya miradi ambayo zabuni yake itatangazwa kwa kadri ya upatikanaji wa fedha. (Makofi)