Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 9 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 146 2022-09-23

Name

Francis Leonard Mtega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbarali

Primary Question

MHE. FRANCIS L. MTEGA aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kuboresha Hifadhi ya Taifa Kitulo?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii naomba kujibu swali la Mheshimiwa Francis Leonard Mtega, Mbunge wa Mbarali kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Hifadhi ya Taifa Kitulo ni hifadhi ya kipekee ambayo huwezi kuifanananisha na hifadhi nyingine hapa nchini. Hifadhi hii ina utalii wa maua, maporomoko ya maji, ndege wa aina mbalimbali na vivutio vingine. Wizara kwa kutambua hilo imeendelea kuboresha miundombinu ndani ya hifadhi. Miundombinu hiyo ni pamoja na kuimarisha barabara zilizomo ndani ya hifadhi, kuanzisha huduma za malazi na chakula, kuongeza mazao mapya ya utalii ndani ya hifadhi kama vile utalii wa kutumia baiskeli, utalii wa kutembea kwa miguu na utalii wa kupanda vilima.

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kutangaza fursa za uwekezaji zilizopo ndani ya hifadhi hiyo ikiwemo maeneo ya malazi na shughuli za utalii kama vile utalii wa farasi, utalii wa kubembea na kamba na mazao mengine ya utalii ili kuongeza idadi ya watalii na idadi ya siku za kukaa hifadhini na hivyo kuongeza mapato zaidi.