Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 20 Works, Transport and Communication Ofisi ya Rais TAMISEMI. 168 2016-05-16

Name

Albert Ntabaliba Obama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buhigwe

Primary Question

MHE. ALBERT O. NTABALIBA aliuliza:-
Mheshimiwa Rais aliahidi ujenzi wa barabara ya Mnanila – Kasulu yenye urefu wa kilometa 42 kwa lami.
(a) Je, lini barabara hiyo itaanza kujengwa?
(b) Zile kilometa nne ambazo Mheshimiwa Rais aliahidi kwamba zingeanza kujengwa kwa kiwango cha lami katika Makao Makuu ya Wilaya ya Buhigwe utaanza lini?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Albert Ntabaliba Obama, Mbunge wa Buhigwe, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Mnanila – Kasulu yenye urefu wa kilometa 48 ni barabara ya mkoa chini ya Wakala wa Barabara Nchini (TANROADS) na inaunganisha Wilaya tatu za Kasulu, Buhigwe, Kigoma na nchi jirani ya Burundi. Barabara hii ni sehemu ya barabara ya Kibondo – Kasulu – Manyovu yenye urefu wa kilometa 250 ambayo kazi ya usanifu wa kina inaendelea ikiwa ni hatua muhimu katika ujenzi kwa kiwango cha lami. Utekelezaji utafanyika kupitia wahisani wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) chini ya Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki. Baada ya kukamilika kwa usanifu, taratibu za ujenzi kwa kiwango cha lami zitafuata.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu ujenzi wa kipande cha barabara kilometa mbili katika makao makuu ya Wilaya ya Buhigwe, Halmashauri imepanga kufanya upembuzi yakinifu na usanifu ambao utasaidia kujua gharama za ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami. Kukamilika kwa hatua hiyo, kutawezesha Serikali kuweka katika mpango na kutenga bajeti ili kuanza ujenzi.