Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 9 Youth, Disabled, Labor and Employment Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu 134 2022-09-23

Name

Anastazia James Wambura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANASTAZIA J. WAMBURA aliuliza: -

Je, ni lini wastaafu ambao waajiri wao walikuwa hawatoi michango katika Mifuko ya Hifadhi ya Jamii watalipwa haki zao?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA NA VIJANA (MHE. PASCAL P. KATAMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Anastazia James Wambura, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mafao ya pensheni hulipwa kwa mstaafu kwa kuzingatia kipindi kilicholipiwa michango yake. Kumekuwepo na changamoto kwa baadhi ya waajiri kushindwa kuwasilisha michango ya watumishi wao katika Mifuko ya Hifadhi ya Jamii kwa wakati. Kutokana na changamoto hiyo, mifuko imekuwa ikichukua hatua mbalimbali ikiwemo kuwapeleka Mahakamani waajiri ambao hawawasilishi michango kwa wakati ili kuwezesha wastaafu hao kupata haki yao.

Mheshimiwa Spika, hatua zilizochukuliwa na mifuko kukabiliana na changamoto hii ni pamoja na kutoa elimu kwa waajiri, kutengeneza namba ya kumbukumbu ya malipo (control number) kupitia Mfumo wa Malipo ya Serikali (GePG) na kupunguza tozo zinazotokana na ucheleweshwaji wa michango hiyo. Aidha, mifuko imeingia makubaliano maalum na waajiri 63 ya namna ya kulipa madeni yao.

Mheshimiwa Spika, waajiri ambao wameendelea kukaidi kuwasilisha michango ya wanachama kwa wakati, Mfuko kwa kushirikiana na Wakili Mkuu wa Serikali (Solicitor General) imechukua hatua ya kuwapeleka Mahakamani kwa mujibu wa sheria. Aidha, waajiri 123 tayari wamefikishwa Mahakamani, ahsante.