Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 20 Health and Social Welfare Ofisi ya Rais TAMISEMI. 167 2016-05-16

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Primary Question

MHE. KEMILEMBE J. LWOTA (K.n.y MHE. STANSLAUS S. MABULA) aliuliza:-
Hospitali ya Wilaya ya Nyamagana inahudumia zaidi ya wakazi 300,000 wakiwemo wanaotoka Wilaya za jirani lakini haina vifaa tiba kama vile x-ray, ultrasound na kadhalika huku ikiwepo ahadi ya Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne mwaka 2013 lakini mpaka sasa ahadi hiyo haijatekelezwa.
Je, ni lini sasa ahadi hiyo itatekelezwa na kuipatia hospitali hiyo vifaa tiba vya kutosha ili kuokoa maisha ya watu wengi wanaopoteza maisha kwa sababu ya kukosa huduma hizo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Stanslaus Mabula, Mbunge wa Nyamagana, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuzingatia umuhimu wa mashine ya x-ray katika utoaji wa huduma za afya, Halmashauri ya Jiji la Mwanza katika bajeti ya mwaka wa fedha 2016/2017 imetenga shilingi milioni 133.14 kwa ajili ya ununuzi na kufunga mashine ya x-ray katika Hospitali ya Nyamagana. Aidha, ultrasound ipo katika hospitali hiyo na inafanya kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri pia katika mwaka wa fedha 2016/2017 imetenga shilingi milioni 33.9 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba kwenye vituo mbalimbali vya afya vinavyotoa huduma za afya ndani ya Wilaya ikiwemo Hospitali ya Wilaya ya Nyamagana. Aidha Halmashauri imetenga shilingi milioni 10.5 kwa ajili ya matengenezo ya vifaa vya hospitali.