Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 1 Foreign Affairs and International Cooperation Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki 16 2022-09-13

Name

Ng'wasi Damas Kamani

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NG’WASI D. KAMANI aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kutumia Balozi zetu kuhakikisha Vijana wengi wa Kitanzania wanaajiriwa nje ya nchi?

Name

Amber. Mbarouk Nassor Mbarouk

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ng’wasi Damasi Kamani, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeweka mkakati maalum wa kuhakikisha kuwa vijana wa Kitanzania wenye sifa zilizowekwa wanapata fursa za ajira nje ya nchi kama ifuatavyo: -

i) Balozi zetu nje ya nchi zimeendelea kutafuta fursa za ajira mbalimbali kwenye maeneo yao ya uwakilishi kwa kuingia mikataba ya ajira nje ya nchi inayowawezesha vijana wetu kupata ajira na kuwahakikishia usalama na maslahi yao katika ajira hizo.

ii) Serikali kupitia Kanzi Data ya Wakala wa Huduma za Ajira Tanzania (TAESA) inawawezesha vijana na wataalam mbalimbali kujiandikisha ili kuwasadia kuomba nafasi za ajira pindi zinapopatikana nje ya nchi.

iii) Wizara inafuatilia nafasi za ajira ambazo hutangazwa katika Jumuiya za Kikanda na Kimataifa na kuziwasilisha katika mamlaka mbalimbali ili kusaidia kuwatambua vijana ambao wanazo sifa kutoka Serikalini na Sekta Binafsi na kuwashawishi kuomba nafasi hizo. Ahsante sana.