Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 8 Sitting 1 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 7 2022-09-13

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE aliuliza: -

Je ni lini Serikali italeta Bungeni Muswada wa Sheria ya Kampuni Binafsi za Ulinzi?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Athuman Almasi Maige, Mbunge Wa Tabora Kaskazini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa kuwepo kwa Sheria inayosimamia Makampuni Binafsi ya Ulinzi na kwa sasa Waraka wa Baraza la Mawaziri kuhusu mapendekezo ya kutunga Sheria ya Huduma za Sekta Binafsi ya Ulinzi umekamilika na utawasilishwa katika Baraza la Mawaziri kwa ajili ya maamuzi baada ya kupata maoni ya kina ya wadau wa pande zote mbili za Muungano juu ya rasimu ya sheria hiyo. Baada ya kukamilika kwa hatua hizo Muswada wa Sheria hiyo utaletwa Bungeni.