Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 14 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 163 2022-02-18

Name

Angelina Adam Malembeka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA aliuliza: -

Fursa zimetolewa kwa watu binafsi kuanzisha ranchi, mashamba na bustani za wanyamapori?

Je, ni wanyama wa aina gani wanaruhusiwa kufugwa na utaratibu gani unaotumika kuwapata na Serikali ina mkakati gani kuhakikisha wanyama hao hawasafirishwi kwenda nje ya nchi?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii naomba kujibu swali la Mheshimiwa Angelina Adam Malembeka, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ufugaji wanyamapori katika ranchi, mashamba na bustani za wanyamapori unasimamiwa na Sheria ya Kuhifadhi Wanyamapori Na. 5 ya mwaka 2009 na Kanuni za Usimamizi wa Maeneo ya Ufugaji Wanyamapori za mwaka 2020. Kwa yeyote anayehitaji kufuga atapaswa kuwa na leseni inayotolewa na Kamishna wa Uhifadhi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) kwa kufuata vigezo vilivyowekwa.

Mheshimiwa Spika, wanyamapori aina zote wanaruhusiwa kufugwa kwa kuzingatia vigezo vilivyowekwa mfano, aina ya mnyamapori, ukubwa wa eneo, na upatikanaji wa chakula na bei zake zimeainishwa katika jedwali la sita la Kanuni za Usimamizi wa Maeneo ya Ufugaji Wanyamapori za mwaka 2020.

Mheshimiwa Spika, kutokana na Tamko la Serikali lililotolewa katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tarehe 25 Mei, 2016 kuhusu zuio la biashara ya usafirishaji wa wanyamapori hai nje ya nchi, leseni zote zinazohusu usafirishaji wa wanyamapori hai nje ya nchi zilizuiliwa.

Aidha, ulinzi katika malango ya kutokea ikiwa ni viwanja vya ndege, bandari, barabara na mipaka ya nchi umeimarishwa ili kuhakikisha hakuna wanyamapori au nyara inayosafirishwa bila kibali ama leseni. Ahsante. (Makofi)