Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 13 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 150 2022-02-17

Name

Sebastian Simon Kapufi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Mjini

Primary Question

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Vituo vya Afya eneo la Nsemulwa na Mwamkulu katika Manispaa ya Mpanda?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Sebastian Simon Kapufi, Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika Mwaka wa Fedha 2021/ 2022 Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda imetenga fedha kiasi cha shilingi milioni 400 kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya Nsemulwa ambapo hadi kufikia Februari, 2022 shilingi milioni 250 zimeshatolewa. Ujenzi wa majengo matatu ya wagonjwa wa nje, maabara na wodi ya wazazi unaendelea.

Mheshimiwa Spika, Serikali imepeleka fedha shilingi milioni 250 katika Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya Mwamkulu ambapo ujenzi wa jengo la OPD umefikia hatua ya lenta na maabara umefikia hatua ya umaliziaji.