Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 12 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 143 2022-02-16

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itamaliza mgogoro wa muda mrefu wa ardhi kati ya TFS/TANAPA na wananchi wa Kata za Inyala, Itewe na Ilungu?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Oran Manase Njeza, Mbunge wa Jimbo la Mbeya Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Hifadhi ya Taifa Kitulo haina mgogoro na vijiji vya Kata za Inyala, Itewe na Ilungu. Changamoto iliyopo ni kuongezeka kwa mahitaji ya ardhi kwa wananchi wa maeneo hayo kwa ajili ya kufanya shughuli za kiuchumi. Maeneo hayo yalikuwa yanatumiwa kinyume cha sheria kwani kwa eneo ambalo ni Hifadhi ya Taifa Kitulo lilikuwa ni shamba la Serikali la mifugo ambamo ndani yake kulikuwa na (ng’ombe na kondoo wa sufu) lililojulikana kama Kitulo Dairy Farm.

Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na kuongezeka kwa uhitaji wa ardhi zaidi, wananchi wamekuwa wakidai maeneo waliyo kuwa nayo wanatumia kabla ya Hifadhi ya Taifa Kitulo kuanzishwa mwaka 2005 yarudishwe kwao ili kukidhi mahitaji zaidi ya ardhi kwa ajili ya shughuli za kilimo na ufugaji. Kutokana na hali hiyo, Serikali kupitia Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) imekuwa ikichukua hatua mbalimbali ikiwemo kuwaelimisha wananchi juu ya umuhimu wa uhifadhi na hifadhi za mazingira kwa ujumla ili kutatua changamoto hiyo.