Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 12 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 136 2022-02-16

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI aliuliza: -

Je, Serikali inaweza kutoa tathmini ya urejeshwaji wa mikopo inayotolewa na Halmashauri kwa Vikundi vya Akinamama, Vijana, na Watu Wenye Ulemavu katika kipindi cha angalau miaka mitatu iliyopita?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Charles Stephen Kimei, Mbunge wa Jimbo la Vunjo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali katika mwaka wa fedha 2018/2019, ilitoa mikopo kiasi cha shilingi bilioni 42.06 ambacho kiasi cha shilingi bilioni 12.88 kilirejeshwa sawa na aslimia 3.6; Mwaka wa fedha 2019/2020 kiasi cha shilingi bilioni 40.73 kilitolewa ambapo kiasi cha shilingi bilioni 14.65 kilirejeshwa sawa na asilimia 35.96; na katika mwaka wa fedha 2020/2021 kiasi cha shillingi bilioni 53.81 kilitolewa ambapo shilingi bilioni 29.85 kilirejeshwa sawa na asilimia 55.47.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeshasanifu mfumo wa kieletroniki utakaowezesha usimamizi madhubuti wa mikopo katika usajili wa vikundi, utengaji wa fedha, utoaji wa mikopo, usimamizi wa marejesho na shughuli za vikundi katika Mamlaka za Serikali za Mitaa. Aidha, mwongozo wa usimamizi wa mikopo hii umeshaandaliwa na upo kwenye hatua za mwisho za uidhinishaji.