Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 11 Works, Transport and Communication Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari 132 2022-02-15

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza: -

Je, ni lini Mtambo wa matangazo ya TBC Taifa na TBC FM utafungwa katika Mji wa Itigi ili Wananchi wapate matangazo hayo muhimu?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Yahaya Omary Massare Mbunge wa Manyoni Magharibi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenekiti, Serikali kupitia Shirika lake la Utangazaji la Taifa (TBC) mkakati wake ni kuhakikisha wananchi wote wanapata huduma ya matangazo ya redio nchi nzima ifikapo Mwaka 2025.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika bajeti ya Mwaka 2022/2023 TBC imepanga kuwasilisha maombi katika Bunge lako tukufu kuidhinishiwa kiasi cha shilingi bilioni saba zitakazotumika mahsusi kwa ajili ya upanuzi wa usikivu katika Wilaya 14 nchini ikiwemo Wilaya ya Manyoni. Mkakati ni kuhakikisha kuwa wananchi wanaoishi katika wilaya ambazo hazipati matangazo ya TBC Taifa na TBC FM zinapata ifikapo mwaka 2025.

Mheshimiwa Mwenekiti, TBC imeendelea kuboresha usikivu katika maeneo ambayo hayana usikivu ama usikivu wake ni hafifu. Miradi inayotekelezwa kwa Mwaka wa fedha 2021/2022 ni katika Wilaya na maeneo 24 ya nchi ikiwemo maeneo ya mpakani ambayo ni Ngara, Karagwe, Kasulu, Tanganyika, Same na Nkasi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maeneo mengine ni Kilombero/Mlimba, Kahama, Sikonge, Bunda, Ngorongoro, Uvinza, Makete, Ruangwa, Kyela, Morogoro Vijijini/Kisaki, Kilwa, Serengeti, Songwe, Njombe, Simiyu, Unguja na Pemba. Miradi hii iko katika hatua mbalimbali za utekelezaji na inatarajiwa kukamilika yote na kuzinduliwa ifikapo Julai, 2022. Miradi hii ikikamilika usikivu wa TBC utafikia asilimia 83, ahsante sana. (Makofi)