Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 11 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 125 2022-02-15

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali italeta Muswada Bungeni ili kuboresha Sheria ya Usalama Barabarani ya mwaka 1973 kutokana na Sheria hiyo kupitwa na wakati?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Rashid Abdallah Shangazi, Mbunge wa Mlalo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua umuhimu wa kupitia na kuboresha Sheria ya Usalama Barabarani ya mwaka 1973. Maboresho ya sheria hiyo yamefanyika ambapo muswada wenye marekebisho hayo ulisomwa kwa mara ya kwanza katika Mkutano wa Tatu wa Bunge la Kumi na Mbili, tarehe 30 Juni, 2021. Muswada huo uliwasilishwa kwenye Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama tarehe 17 Agosti, 2021 ambapo ushauri na maoni ya Kamati yalizingatiwa. Hatua inayofuata ni kufikishwa Bungeni ili kusomwa kwa mara ya pili na tatu hatimaye kuridhiwa.