Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 11 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 124 2022-02-15

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Primary Question

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA aliuliza: -

Je, kwa mwaka 2018 hadi 2021 ni walemavu wangapi wenye sifa husika wameajiriwa katika nafasi zilizotolewa na Serikali, na ni sawa na asilimia ngapi ya watu wenye ulemavu wenye sifa hizo nchini?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, (MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Eng. Stella Martin Manyanya, Mbunge wa Nyasa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kipindi cha kuanzia mwaka 2018 hadi 2021 Serikali imeajiri watumishi wenye ulemavu wapatao 312 wenye sifa stahiki katika fani mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa takwimu zilizopo za wahitimu wenye ulemavu ambao wamejiorodhesha katika kanzidata ya Serikali inaonesha kwamba, kuanzia mmwaka 2018 hadi 2021 wahitimu wenye ulemavu walioajiriwa katika utumishi wa Umma ni asilimia 56 ya wahitimu wenye ulemavu waliopo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda kutoa rai na kusisitiza wahitimu wenye ulemavu wenye sifa za elimu na taaluma mbalimbali ambazo zipo ndani ya utumishi wa Umma kuomba kazi pindi zinapotangazwa ili waweze kuajiriwa katika utumishi wa Umma kwani ajira hutolewa kwa usawa na kwa watu wote wenye sifa zinazohitajika katika nafasi husika pamoja na kuzingatia ujumuishaji wa watu wenye ulemavu. Vile vile, nitumie fursa hii kuwakumbusha waajiri wote kuzingatia ujumuishwaji wa watu wenye ulemavu katika ajira zote zinazotangazwa na Serikali kwa mujibu wa Sheria ya Watu Wenye Ulemavu Na. 9 ya Mwaka 2010.