Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 10 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 109 2022-02-14

Name

Benaya Liuka Kapinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga daraja linalounganisha Vijiji vya Kingoli – Litumbandyosi Wilaya ya Mbinga na Machimavyalafu Wilaya ya Ludewa katika Mto Ruhuhu?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Liuka Kapinga Benaya, Mbunge wa Jimbo la Mbinga Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, daraja la kuunganisha Vijiji vya Kingoli – Litumbandiyosi ni moja kati ya madaraja makubwa ambayo yamepewa kipaumbele na Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Kingoli hadi mto Ruhuhu yenye urefu wa kilometa 13.0 kwa sasa haipitiki kutokana na kukosekana kwa madaraja madogo ya kudumu katika Mito ya Linyanya na Nyamilola pamoja na daraja kubwa la Mto Ruhuhu. Hata hivyo, TARURA Wilaya ya Mbinga, ilitenga fedha katika Bajeti ya Mwaka wa fedha 2021/2022 ili kujenga madaraja mawili madogo ya Linyanya na Nyamilola na sasa hivi mkandarasi yuko anaendelea na kazi ya ujenzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na uhitaji mkubwa wa madaraja katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga na kwa kuzingatia umuhimu wa daraja linalounganisha Mkoa wa Ruvuma na Njombe kupitia vijiji vya Kingoli – Litumbandiyosi, Serikali kupitia Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini itatenga shilingi milioni 25 katika bajeti ya mwaka wa fedha 2022/2023 kwa ajili ya kufanya usanifu wa daraja linalounganisha Mikoa ya Ruvuma na Njombe lisilopungua urefu wa mita 40 ili kujua gharama halisi na ujenzi wake utaanza kulingana na upatikanaji wa fedha kuanzia bajeti ya mwaka wa fedha 2023/2024. Ahsante.