Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 10 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 108 2022-02-14

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. DEO K. SANGA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itakamilisha ahadi ya Mheshimiwa Rais ya kujenga kilomita sita ya barabara kwa kiwango cha lami katika Mji wa Makambako?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Deo Kasenyenda Sanga, Mbunge wa Jimbo la Makambako, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara zilizoahidiwa zinasimamiwa na Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini kwa maana ya TARURA. Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Tano aliahidi kujenga kilomita sita za barabara kwa kiwango cha lami katika Halmashauri ya Mji wa Makambako ambapo Wakala wa Barabara TANROADS alikasimiwa kutekeleza ujenzi huo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hadi kufikia mwaka wa fedha 2020/2021, jumla ya kilomita 3.5 zimejengwa kwa kiwango cha lami ambapo jumla ya Shilingi bilioni 1.97 zilitumika katika ujenzi huo. Aidha, Serikali itaendelea kutenga fedha ili kukamilisha ujenzi wa kilomita sita kwa kiwango cha lami kwa kadri fedha zitakavyopatikana. Ahsante sana.