Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 9 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 100 2022-02-11

Name

Norah Waziri Mzeru

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NORAH W. MZERU aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuufanya Mkoa wa Morogoro kuwa moja ya kitovu kikuu cha utalii duniani kwa kuwa ni Mkoa wenye vyanzo vingi vya utalii?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Norah Waziri Mzeru, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika kuongeza kasi ya ukuaji wa sekta ya utalii katika Mkoa wa Morogoro, Serikali ilipandisha hadhi sehemu ya Pori la Akiba la Selous kuwa Hifadhi ya Taifa ya Nyerere. Sambamba na jitihada hizo, Serikali kupitia Mradi wa Kukuza Maliasili na Kuendeleza Utalii (REGROW), barabara zenye urefu wa takribani kilometa 996, njia za watembea kwa miguu kilometa 132.5, viwanja vya ndege saba, malango ya kuingilia wageni nane, vituo vya askari nane na vituo vya kutolea taarifa kwa wageni vitatu vitajengwa katika Hifadhi za Taifa za Mikumi, Udzungwa na Nyerere Mkoani Morogoro. Juhudi hizi zitaendelea kuchochea hali ya utalii katika Mkoa huo.

Mheshimiwa Spika, sambamba na hilo katika hatua nyingine Serikali imeendelea kupandisha hadhi maeneo mbalimbali ikiwemo Hifadhi ya Wanyamapori ya Jamii ya Wami Mbiki kuwa Pori la Akiba. Vilevile kukamilika kwa reli ya mwendokasi (SGR) pamoja na kutumika kwa reli ya TAZARA kutaongeza wigo wa shughuli za utalii katika mikoa ya Morogoro na Pwani. (Makofi)