Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 9 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 92 2022-02-11

Name

Hamida Mohamedi Abdallah

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Lindi Mjini

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatoa fedha za ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Lindi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) Alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hamida Mohamed Abdallah, Mbunge wa Jimbo la Lindi Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali imetenga kiasi cha shilingi bilioni 2.7 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa Hospitali mpya ya Rufaa ya Mkoa wa Lindi. Mara baada ya kukamilika kwa ujenzi huo na kuanza kutoa huduma, miundombinu ya Hospitali ya Rufaa ya sasa itakuwa Hospitali ya Halmashauri ya Manispaa ya Lindi.

Mheshimiwa Spika, ili kuendelea kuimarisha na kuboresha huduma za afya kwa wananchi Serikali tayari imekwishaipatia Halmashauri ya Manispaa ya Lindi, shilingi milioni 500 kwa ajili ya kujenga kituo cha afya kwenye eneo la Kimkakati na lenye mahitaji makubwa. Ahsante. (Makofi)