Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 7 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 76 2022-02-09

Name

Tumaini Bryceson Magessa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami barabara ya kutoka Geita kupitia Nyarugusu kwenda Bukoli hadi Kahama ambapo upembuzi yakinifu ulishafanyika?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Bryceson Magesa Tumaini, Mbunge wa Busanda, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina na kuandaa nyaraka za zabuni kwa barabara ya Geita – Nyarugusu – Kahama yenye urefu wa kilometa 133.9 imekamilika mwaka 2017. Kwa sasa Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami. Aidha, mwaka 2021, Kampuni ya Uchimbaji Madini ya Barrick ilionesha nia ya kufadhili ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami. Kwa sasa, Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi (Sekta ya Ujenzi), Ofisi ya Rais (TAMISEMI), Wizara ya Madini na Wizara ya Fedha na Mipango zinaendelea na mazungumzo na Kampuni ya Barrick kuhusu utaratibu wa ujenzi wa barabara hii.

Mheshimiwa Spika, wakati ujenzi kwa kiwango cha lami ukisubiri upatikanaji wa fedha, Serikali kupitia Wakala wa Barabara (TANROADS), inaendelea kuifanyia matengenezo mbalimbali barabara hii ili iendelee kupitika majira yote ya mwaka. Katika mwaka wa fedha 2021/2022, jumla ya shilingi milioni 838.97 zilitengwa kwa ajili ya matengenezo mbalimbali katika barabara hii. Aidha, Wakala wa Barabara nchini (TANROADS) Shinyanga kwa kutumia fedha za maendeleo inakamilisha ujenzi wa mita 600 kwa kiwango cha lami katika barabara hii kuanzia eneo la Busoka katika Manispaa ya Kahama. Ahsante. (Makofi)