Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 7 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 74 2022-02-09

Name

Dennis Lazaro Londo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. DENNIS L. LONDO aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha Bwawa la Zombo linatumika kikamilifu kwa ufugaji wa samaki na kuondoa tatizo la ajira kwa vijana?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi naomba kujibu swali la mheshimiwa Dennis Lazaro Londo, Mbunge wa Mikumi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kushirikiana na Mamlaka ya Serikali za Mitaa ina mpango endelevu wa kufanya tathmini ya mabwawa yaliyopo katika halmashauri mbalimbali nchini ili kufahamu uwekezaji unaofaa kwenye bwawa husika kulingana na jiografia ya eneo hilo. Kwa kuwa shughuli hii ni endelevu na hufanyika kwa awamu, Bwawa la Zombo litaingia kwenye mpango wa tathmini katika mwaka wa fedha 2022/2023 ili kujua aina ya uwekezaji unaofaa katika Bwawa hilo.

Mheshimiwa Spika, vile vile, wataalam wa Kituo cha Ukuzaji Viumbe Maji cha Kingolwira – Morogoro watatoa mafunzo maalum ya ufugaji samaki kwa vijana wa Jimbo la Mikumi ili kuwapa stadi za ufugaji samaki wenye tija kwenye mabwawa kwa lengo la kutengeneza ajira. ahsante.