Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 6 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 64 2022-02-08

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Tabora – Mambali – Ishihimulwa – Shitage – Muhulidede kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Athuman Almas Maige, Mbunge wa Tabora Kaskazini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Barabara ya Tabora – Mambali – Bukumbi – Ishihimulwa – Shitage – Muhulidede yenye urefu wa kilomita 109.4 ni sehemu ya barabara inayounganisha mikoa ya Tabora na Shinyanga. Sehemu ya barabara kutoka Tabora hadi Bukumbi yenye urefu wa kilometa 84 ni barabara ya mkoa. Kutoka Bukumbi hadi Muhulidede yenye urefu wa kilometa 25.4 ni barabara ya wilaya iliyokasimiwa kwa Wakala wa Barabara (TANROADS) kuanzia mwaka wa fedha 2018/2019.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sehemu ya barabara hii kutoka Tabora hadi Mambali yenye urefu wa kilomita 56, imefanyiwa usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami. Kazi ya usanifu ilikamilika mwezi Aprili, 2020. Baada ya kukamilika kwa usanifu na gharama za ujenzi kujulikana, Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuanza kazi za ujenzi kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sehemu ya barabara iliyobaki ya kutoka Mambali – Bukumbi hadi Muhulidede yenye urefu wa kilomita 53.4, Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuifanyia upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi wa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kuhakikisha kuwa barabara hii ya Tabora - Mambali – Bukumbi hadi Muhulidede inapitika vizuri majira yote, katika mwaka wa fedha 2021/2022, jumla ya Shilingi milioni 443.989/= zimetengwa kwa ajili ya kuifanyia matengenezo mbalimbali. Ahsante.