Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 6 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 59 2022-02-08

Name

Francis Leonard Mtega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbarali

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI K.n.y. MHE. FRANCIS L. MTEGA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itakamilisha kuvipatia umeme wa REA Vitongoji na Vijiji vilivyobaki katika Jimbo la Mbarali?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Francis Leonard Mtega, Mbunge wa Mbarali, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Mbarali ina jumla ya vijiji 102. Ni vijiji 20 tu ambavyo bado havijapatiwa umeme. Vijiji hivyo 20 vinapatiwa umeme kupitia Mradi wa REA mzunguko wa Pili awamu ya Tatu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mradi huu unaendelea kutekelezwa na Mkandarasi ambaye ni M/S Electrical Transmission and Distribution Construction and Maintenance Co. LTD. Mkandarasi amekamilisha kazi ya usanifu wa kina, upimaji, uandaaji wa michoro na anaendelea na manunuzi ya vifaa pamoja na kusimika nguzo katika maeneo ya mradi. Gharama ya mradi ni Shilingi bilioni saba na utekelezaji unatarajiwa kukamilika mwezi Desemba, 2022.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa vitongoji, Serikali imeshaanza utekelezaji wa miradi ya ujazilizi unaolenga kufikisha umeme katika vitongoji vyote Tanzania Bara awamu kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha ikiwa ni pamoja na Vitongoji vya Jimbo la Mbarali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hatua nyingine, Serikali imefanya uhakiki na kuainisha uwepo wa vitongoji takribani 37,610 visivyokuwa na umeme Tanzania Bara na inakadiriwa takribani shilingi trilioni saba zitahitajika ili kukamilisha mahitaji ya umeme katika vitongoji hivyo vyote.