Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 54 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 469 2016-06-30

Name

Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. MENDRAD L. KIGOLA aliuliza:-
Jimbo la Mufindi Kusini linazungukwa na msitu wa Serikali na vijana wanaishi humo hawana ajira.
(a) Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwapa vibali vya kupasua mbao ili kwa kazi hiyo wajiajiri?
(b) Je, Serikali haioni haja ya kuwapa vijana hao mtaji ili waanzishe viwanda vidogo vya mbao?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mendrad Lutengano Kigola, Mbunge wa Mufindi Kusini, lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Jimbo la Mufindi Kusini linapakana na msitu wa shamba la miti la Sao Hill ambalo ni miongoni mwa mashamba ya misitu ya kupandwa 18 nchini. Upasuaji wa mbao ni sehemu moja tu ya mchakato mzima wa uvunaji wa mazao ya misitu unaotekelezwa na Wizara yangu kwa mujibu wa mwongozo wa uvunaji endelevu na biashara ya mazao ya misitu yanayovunwa katika mashamba ya miti na misitu ya mikoko kwa mwaka 2014, chini ya Sheria ya Misitu namba 14 ya mwaka 2002 na Sera ya Taifa ya Misitu ya mwaka 1998. Mwongozo huo umeweka vipaumbele mbali mbali katika uvunaji wa mazao ya misitu ikiwemo vikundi vya vijana.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kutambua changamoto za kiuchumi na kijamii kwa vijana katika maeneo husika Serikali imekuwa ikishirikiana na umoja wa vikundi vya kijamii Wilayani Mufindi kwa kuwapatia vibali kwa ajili ya kuwezesha kupata mitaji ili kuwekeza katika miradi mingine ya kiuchumi. Kwa miaka mitatu mfululizo 2013/2014 hadi 2015/2016 vijana kupitia umoja huo wamekuwa wakigawiwa mita za ujazo 200 kila mwaka. Fedha inayotokana na vibali hivi huratibiwa na umoja wao, na imewawezesha kuanzisha shughuli mbalimbali ikiwemo kununua mizinga ya ufugaji nyuki, ufugaji wa ng’ombe wa maziwa, ufugaji wa kukuna hata mitaji kwa ajili ya biashara ndogo ndogo.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kuhakikisha uwezeshaji wa vijana wanaoishi jirani na msitu kwa namna endelevu, shamba la miti Sao Hill hutoa miche ya miti kwa ajili ya kupanda kwenye mashamba wanayomiliki wenyewe ili waweze kuvuna na kuuza mbao na kujipatia mfanikio ya kiuchumi na kijamii ikiwemo upatikanaji wa ajira. Kwa mfano katika mwaka 2015/2016 shamba lilitoa bure miche 600,000 yenye thamani isiyopungua shilingi 120,000,000 kwa ajili ya kuwawezeshavijana hao.
Aidha, ili kuhakikisha kuwa jamii inanufaika na uwepo wa shamba hilo na kuwapunguzia adha ya michango kwa shughuli za maendeleo vijiji vinavyozunguka shamba hilo vinapatiwa vibali vya kuvuna miti kwa ajili ya shughuli za kimaendeleo ikiwemo kutengeneza madawati, kazi ambayo pia hupewa mafundi ambao ni vijana wanaishi katika vijiji vinayozunguka shamba hilo. Kwa mfano, katika kipindi cha mwaka 2011/2012 hadi 2014/2015 jumla ya meta za ujazo 40,000 zilitolewa kwa vijiji vya jirani na kwa mwaka 2013/2014 pekee baadhi ya vijiji vilitumia mgao huo kutengeneza jumla ya madawati 2,469.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara yangu inatoa ushauri kwa vijana kuungana pamoja na kuunda ushirika ambao utawezesha kupata mikopo kutoka taasisi mbalimbali za fedha na hatimaye kujenga uwezo wa kuendesha shughuli zao za kila siku ikiwa ni pamoja na kuwekeza katika viwanda vya mbao yaani saw mills ili waweze kuomba vibali vya uvunaji kajadiliwa kama wateja wengine wenye viwanda.