Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 5 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 53 2022-02-07

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. FESTO R. SANGA aliuza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kutekeleza Mradi wa REA katika Wilaya ya Makete ili kuhakikisha umeme unafika kila Kijiji?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Festo Richard Sanga, Mbunge wa Makete, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Makete ina jumla ya vijiji 93 na vijiji 56 vimekwisha fikishiwa umeme. Vijiji 37 ambavyo havikuwa na umeme vinapatiwa umeme kupitia Mradi wa REA awamu ya III, mzunguko wa pili unaoendelea kutekelezwa na Mkandarasi M/S JV Silo Power Limited na Guangzhou Yidian Equipment Installation Company Limited. Mkandarasi anaendelea na kazi ya usanifu wa kina, upimaji, uandaaji wa michoro na manunuzi ya vifaa.

Mheshimiwa Spika, Mradi wa kupeleka umeme katika Wilaya ya Makete unahusisha ujenzi wa njia ya umeme ya msongo kilovoti 33, zenye urefu wa kilomita 222.5; kilomita 37 ya njia ya umeme ya msongo wa kilovoti 0.4; ufungwaji transfoma 37 za KVA 50; pamoja na kuunganisha wateja wa awali 814. Gharama ya mradi ni Shilingi bilioni 9.95 na utekelezaji unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Desemba, 2022.