Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 5 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 50 2022-02-07

Name

Yustina Arcadius Rahhi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. YUSTINA A. RAHHI aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuchimba malambo kwa ajili ya maji ya mifugo katika maeneo ya wafugaji mkoani Manyara?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Yustina Arcadius Rahhi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2020/ 2021, Serikali imekamilisha ukarabati wa mabwawa matatu likiwemo bwawa la Narakauo lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara. Aidha, katika mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali itaendelea kutenga fedha za kuchimba mabwawa na visima virefu katika maeneo mbalimbali nchini hususan maeneo yaliyoathirika na ukame ukiwemo Mkoa wa Manyara.

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kuhimiza Mamlaka zote za Serikali za Mitaa nchini kutekeleza Waraka wa Rais Na.1 wa Mwaka 2002, unaozielekeza kutenga fedha kiasi kisichopungua asilimia 15 kwa mapato yatokanayo na mifugo ili zitumike kutekeleza shughuli za Sekta ya Mifugo ikiwemo uchimbaji na ujenzi wa miundombinu ya maji kwa ajili ya mifugo. Aidha, Uboreshaji wa miundombinu hiyo ya mifugo uwe Shirikishi kwa kuwahusisha wafugaji.