Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 5 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 45 2022-02-07

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Primary Question

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE Aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya kuanzia Matai kwenda Kasesya border inayounganisha nchi yetu na nchi ya Zambia?

Name

Prof. Makame Mnyaa Mbarawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkoani

Answer

WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI Alijibu:-

Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Josephat Sinkamba Kandege Mbunge wa Kalambo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Kazi ya Upembuzi yakinifu, Usanifu wa Kina na Uandaaji wa Nyaraka za Zabuni wa Barabara ya Matai - Kasesya yenye urefu wa kilomita 50 imekamilika. Serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) ipo katika hatua za mwisho za manunuzi kwa ajili ya kumpata Mkandarasi wa ujenzi kwa kiwango cha lami wa kilometa 25 sehemu ya Matai – Tatanda ambapo rasimu ya mkataba imepelekwa kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali tarehe 27 mwaka huu kwa ajili ya kupata ridhaa (vetting) ili mkataba uweze kusainiwa. Aidha, Serikali kupitia TANROADS iko kwenye maandalizi ya kutangaza zabuni ya kazi ya ujenzi kwa sehemu iliyobaki ya kutoka Tatanda – Kasesya yenye urefu wa kilometa 25. Zabuni itakuwa imetangazwa kabla ya mwezi Juni mwaka huu.