Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 4 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 38 2022-02-04

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. VITA R. KAWAWA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuwarudishia wamiliki halali silaha zao ambazo zilichukuliwa na Serikali wakati wa zoezi la Operesheni Tokomeza?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MUUNGANO NA MAZINGIRA K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Vita Rashid Kawawa, Mbunge wa Jimbo la Namtumbo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, mnamo mwaka 2013, Serikali baada ya kuona matukio ya ujangili na uwindaji haramu umeongezeka hapa nchini, hasa kwenye hifadhi za Taifa na mapori tengefu, iliendesha Operesheni Tokomeza na lengo lake lilikuwa kuwasaka na kuwakamata majangili pamoja na silaha walizokuwa wakizitumia. Operesheni hiyo ilishirikisha TAWA pamoja na vikosi vya ulinzi na usalama na jumla ya silaha 1,579 zilikamatwa na mpaka sasa zinashikiliwa na Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tarehe 7 Januari, 2017 Serikali kupitia Wizara za Kisekta ambazo ni Wizara ya Maliasili na Utalii, Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi na Wizara ya Katiba na Sheria, walikubaliana kwa pamoja silaha hizo zisirudishwe kwa wamiliki mpaka itakapofanyika tathmini ya hitaji la kuwarejeshea wamiliki wa silaha hizo. Nakushukuru.