Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 4 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 35 2022-02-04

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. CECIL D MWAMBE K.n.y. MHE. BONIPHACE M. GETERE aliuliza: -

(a) Je ni lini mikataba ya miradi mbalimbali ya migodi ya madini, ujenzi wa Bandari Bagamoyo, ujenzi wa Reli (SGR), ujenzi wa Bwawa la Mwalimu Nyerere, Bomba la Mafuta na Mradi wa Bomba la Gesi kutoka Mtwara hadi Dar es Salaam italetwa Bungeni ili kupata ufahamu wa miradi hiyo?

(b) Je, katika mikataba hii ni mingapi imewahi kukaguliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria naomba kujibu swali la Mheshimiwa Boniphace Mwita Getere, Mbunge wa Bunda kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa za mikataba ya ujenzi wa Reli ya SGR, ujenzi wa Bwawa la Mwalimu Nyerere, Migodi ya Madini, Bomba la Mafuta na Mradi wa Bomba la Gesi kutoka Mtwara hadi Dar es Salaam kwa nyakati tofauti Taasisi na Mashirika yanayosimamia miradi hii yamekuwa yakiwasilisha kwenye Kamati za Kudumu za Bunge taarifa za mikataba ya miradi hiyo. Aidha, Kamati zina mamlaka kwa mujibu wa Kanuni za Kudumu za Bunge kupata taarifa zozote kuhusiana na mikataba ya miradi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sehemu ya pili, miradi hii imekuwa ikikaguliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali yaani CAG. Kwa kuwa baadhi ya miradi Serikali inamiliki kwa asilimia 100 na mingine Serikali ni mbia, hivyo taarifa zake huwasilishwa katika Bunge lako tukufu kupitia Ripoti ya CAG. Katika mwaka wa fedha 2019/2020, Sura ya Tano na Sita inabainisha kwa kina taarifa ya ukaguzi ya miradi ya ujenzi wa Reli SGR kwa Lot. 1 na Lot. 2 na Mradi wa Bwawa la Umeme la Mwalimu Nyerere. Aidha, mradi wa Bomba la Gesi kutoka Mtwara hadi Dar es Salaam umekuwa ukifanyiwa ukaguzi wa kawaida kila mwaka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nipende kumuarifu Mheshimiwa Mbunge na pia Bunge lako tukufu kuwa Bunge limekuwa likipokea taarifa za mikataba na Ripoti za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kama nilivyoeleza hapo juu. Ahsante.