Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 4 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 33 2022-02-04

Name

Martha Festo Mariki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI K.n.y. MHE. MARTHA F. MARIKI aliuliza: -

Je, ni lini ujenzi wa barabara za kuunganisha Mkoa wa Katavi na Mikoa ya jirani utaanza?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Martha Festo Mariki, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, utekelezaji wa miradi ya barabara za kuunganisha Mkoa wa Katavi na mikoa jirani ya Kigoma, Rukwa na Tabora ni kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea na jitihada za kuunganisha Mkoa wa Katavi na Mkoa wa Kigoma ambapo ujenzi wa barabara ya Mpanda – Ifukutwa - Vikonge yenye urefu wa kilometa 37.65 umekamilika kwa kiwango cha lami. Aidha, katika mwaka wa fedha 2021/2022 sehemu ya barabara ya Vikonge – Mishamo Junction yenye urefu wa kilometa 62 imetengewa shilingi milioni 3,000 kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami. Aidha, Serikali kupitia TANROADS iko katika hatua za mwisho za mchakato wa zabuni ya kumpata mkandarasi wa ujenzi kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa Mikoa ya Katavi na Rukwa, ujenzi wa sehemu za Sumbawanga – Kanazi urefu wa kilometa 75, Kanazi – Kizi – Kibaoni kilometa 76 na Mpanda – Sitalike kilometa 36.5 kwa kiwango cha lami umekamilika. Katika mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali imetenga shilingi milioni 4,000 kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami barabara ya Kibaoni – Sitalike yenye urefu wa kilometa 71. Serikali kupitia TANROADS iko katika hatua za mwisho za mchakato wa zabuni ya kumpata mkandarasi wa ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile kwa Mikoa ya Katavi na Tabora, utekelezaji wa barabara ya Tabora – Ipole – Koga – Mpanda yenye urefu wa kilometa 359 ni kama ifuatavyo; Tabora – Sikonge yenye urefu wa kilometa 30 ujenzi umekamilika; sehemu ya Usesula – Komanga yenye urefu wa kilometa 108 na barabara ya kuingia Mji wa Sikonge yenye urefu wa kilometa 7.5; sehemu ya Komanga – Kasinde yenye urefu wa kilometa 108 na barabara ya kuingia Mji wa Inyonga kilometa 4.8; sehemu ya Kasinde – Mpanda kilometa 108 na barabara ya kuingia Mji wa Urwira yenye urefu wa kilometa 3.7 ujenzi wake umekamilika. Ahsante. (Makofi)