Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 2 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 11 2022-02-02

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA Aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua changamoto ya upungufu wa Madaktari Bingwa na vifaa tiba katika Hospitali ya Rufaa ya Kitete Mkoani Tabora?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA Alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Afya, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Emmanuel Adamson Mwakasaka, Mbunge wa Tabora Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Hospitali ya Rufaa Kitete ina Madaktari Bingwa watatu wanaotoa huduma ya wanawake na watoto. Pia, Serikali imetoa ufadhili wa masomo kwa Madaktari sita wa hospitali hii ambao wanasomea fani mbalimbali za kibingwa; fani hizo ni Wanawake na Afya ya Uzazi mmoja, Masikio, Pua na Koo mmoja, Magonjwa ya Ndani wawili, Huduma za Dharura mmoja na Mionzi (Radiolojia) mmoja. Madaktari hao wanatarajiwa kuhitimu mwaka wa masomo 2022/2023.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imetoa jumla ya Shilingi Bilioni 10.5 kwa ajili ya ujenzi wa jengo la wagonjwa mahututi (ICU) pamoja na vifaa vyake, jengo la huduma ya mama na mtoto, jengo la dharura (EMD) pamoja na vifaa vyake na ununuzi wa CT-Scan Pamoja na jengo lake ambapo shughuli hizo zote zimeanza.