Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 2 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 9 2022-02-02

Name

Tarimba Gulam Abbas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kinondoni

Primary Question

MHE. TARIMBA G. ABBAS aliuliza: -

Utoaji wa leseni za biashara kwa biashara ndogo za maduka katika Manispaa ya Kinondoni umekuwa na changamoto kutokana na wafanyabiashara hao kutokuwa na Tax Clearence kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Je, ni kwa nini Serikali isiiagize TRA kwenda mitaani na kubaini biashara hizo na kuzisajili kwa lengo la kurahisisha utoaji wa Tax Clearance ili leseni ziweze kutolewa?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango naomba kujibu swali la Mheshimiwa Tarimba Gulam Abbas, Mbunge wa Kinondoni kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, miongoni mwa changamoto zinazopelekea wafanyabiashara kutopatiwa Tax Clearance ambalo ni takwa la kupatiwa leseni ya biashara, ni pamoja na wafanyabiashara hao kutosajiliwa na kupatiwa namba ya utambulisho wa mlipakodi (TIN Number).

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kutatua changamoto hii kwa wafanyabiashara, Serikali imeongeza kasi ya zoezi la usajili wa walipakodi katika jiji la Dar es Salaam na Tanzania kwa ujumla.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Mamlaka ya Mapato Tanzania inaendelea na kampeni ya mlango kwa mlango ili kutatua changamoto zinazowakabili walipakodi ikiwa ni pamoja na kutoa elimu ya kodi, kuwatambua walipakodi wapya na kuwasajili. Lengo la kampeni hii ni kurahisisha zoezi la usajili wa walipakodi kwa kuwasogezea karibu huduma hii wafanyabiashara wote nchini, kwa kuwafuata katika maeneo yao ya biashara badala ya kuwasubiria waje katika Ofisi za Mamlaka ya Mapato Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, zoezi hili maalum limeanza mwezi Agosti, 2021 katika mikoa yote ya kikodi katika Jiji la Dar es Salaam ikiwemo Manispaa ya Kinondoni na litaendelea nchi nzima. Ni matumaini ya Serikali kuwa zoezi hili litaongeza idadi ya walipakodi waliosajiliwa na hivyo kurahisisha upatikanaji wa tax clearance ili leseni za biashara ziweze kutolewa kwa uharaka zaidi. Ahsante.