Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 9 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 92 2021-11-12

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza:-

Ukatili kwa watoto umekithiri nchini kama vile ubakaji, ulawiti, kuchomwa moto na mimba za utotoni.

(a) Je ni watoto wangapi wamefanyiwa ukatili huo kwa jinsia zao wa kike na wa kiume?

(b) Je kuna takwimu halisi ya hatua zilizo chukuliwa na Serikali dhidi ya matukio hayo nchini?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Esther Nicholas Matiko Mbunge Viti Maalum lenye vipengele (a) na (b) kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kuanzia Januari hadi Septemba 2021 takwimu ya vitendo vya ukatili kwa watoto vilivyoripotiwa Vituo vya Polisi inaonyesha jumla ya watoto 6,168 wamefanyiwa ukatili na kati yao wanawake 5,287 na wanaume 881, waliobakwa ni 3,524, waliolawitiwa ni 637 kati yao wanaume 567 na wanawake 70, waliochomwa moto ni 130 kati yao wanaume 33 na wanawake 97, waliopata mimba ni 1,877.

Mheshimiwa Spika, kesi na watuhumiwa waliokamatwa na kufikishwa Mahakamani ni 3,800, kesi zilizo chini ya upelelezi ni 2,368 na kesi zilizohukumiwa ni 88 na nyingine ziko kwenye hatua mbalimbali Mahakamani. Nakushukuru.