Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 9 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 91 2021-11-12

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. CECIL D. MWAMBE aliuliza: -

Je, Serikali imefikia hatua gani katika kutekeleza amri ya Mahakama ya kuwalipa fidia Wanakijiji wanaozunguka katika eneo la Gereza la Namajani?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Napenda Kujibu Swali La Mheshimiwa David Cecil Mwambe Mbunge wa Jimbo la Ndanda lenye vipengele (a) na (b) kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kulikuwepo na mgogoro wa ardhi baina ya Gereza la Namajani na wanakijiji wa Kijiji cha Ngalole. Mgogoro huo ulitatuliwa na Mahakama kwa kuamuru Jeshi la Magereza kulipa fidia ya shilingi bilioni 2.4 kwa eneo la ukubwa wa ekari 2,064 lililokuwa na mgogoro.

Mheshimiwa Spika, katika kutekeleza amri ya Mahakama ya kulipa fidia kwa wanakijiji wanaozunguka eneo la Gereza Namajani, Serikali kwa nia thabiti tayari imefanya utambuzi wa Wanakijiji wanaostahili kulipwa fidia kama hatua za awali na hivi sasa inaendelea na mchakato wa upatikanaji wa fedha za kulipa fidia hiyo na pindi fedha itakapopatikana italipwa haraka kwa wananchi hao.