Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 9 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 90 2021-11-12

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa barabara ya kutoka Kalambo Falls hadi barabara kuu inayokwenda Matai yenye urefu wa kilometa17?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bupe Nelson Mwakang’ata Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mpaka sasa ukarabati wa barabara hiyo yenye urefu wa kilometa 17 kwa kiwango cha Changarawe unaendelea ambapo kwa mwaka wa fedha 2020/2021, Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) kwa Halmashauri ya Wilaya Kalambo kwa kushirikana na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania kwa maana ya TFS ulitumia kiasi cha shilingi milioni 139.72 kukarabati sehemu ya barabara hiyo kipande chenye urefu wa Kilometa 10.

Mheshimiwa Spika, vile vile kwa mwaka wa fedha 2021/2022 Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) Halmashauri ya Wilaya Kalambo umetenga kiasi cha shilingi milioni 84.5 kwa ajili ya matengenezo ya muda maalum kwa maana Periodic Maintenance kipande chenye urefu wa kilometa 4 na Mkandarasi amekwisha patikana na yupo eneo la mradi akiendelea na kazi.

Mheshimiwa Spika, hali ya barabara hii kwa sasa inaridhisha kwani inapitika katika kipindi chote cha mwaka. Aidha, kutokana na umuhimu wa barabara hii, Serikali itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya matengenezo yake kulingana na upatikanaji wa fedha.